TULIKUWA TUNAITAKA SIMBA MWAKA HUU
Na Kambi Mbwana

UONGOZI wa klabu ya Yanga, umesema walikuwa wana hamu ya kukutana na Simba kabla mwaka huu haujamalizika ili waweze kulipiza kisasi cha kufungwa bao 1-0 katika mzunguko wa kwanza wa ligi kuu ya soka Tanzania bara.
Akizungumza jana, Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa Yanga, Lawrence Mwalusako alisema kuwa wamefurahi sana kukutana na Simba katika mchezo wa nusu fainali.
“Tulikuwa tuna hamu kubwa ya kukutana na Simba lakini Mungu ametujalia kukutana na mnyama sasa nawaeleza mashabiki wote wa SImba wafahamu kuwa keshokutwa ni zamu yetu ya kushinda mchezo huo,” alisema Mwalusako
“Tumepania kweli kweli kuifunga Simba katika mchezo huo, hivi sasa tuna kocha mzuri mwenye uwezo wa juu, Kostadin Papic,” alisema.

  Kwa mara ya mwisho, Simba iliifunga Yanga bao 1-0 lilofungwa na mshambuliaji Mussa Hassan ‘Mgosi’ katika kipindi cha kwanza Oktoba 31, mwaka huu.

.

Maoni

Jina

Barua Pepe

 


Logo Logo
||Mtanzania|| Bingwa|| Rai|| Dimba|| The African||
TANGAZA NASI
Click to View National Business Directory Details
Home
Maoni ya Mhariri
Habari za Kitaifa
Habari za Kimataifa
Wazo Binafsi
Makala na Barua
Udhamini
Biashara
Elimu na Jamii
Michezo
Burudani
Directory 2010
Wasiliana Nasi