SHIMUTA KUKUTANA NA BMT, WAZIRI WA HABARI
Na Winfrida Ngonyani
UONGOZI mpya wa Shirikisho la Michezo ya Mashirika ya Umma na Makampuni Binafsi Tanzania, SHIMUTA, liko mbioni kukutana na Baraza la Michezo la Taifa BMT na Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, George Mkuchika, kama njia mojawapo ya kujitambulisha.
Akuzungumza na Mtanzania jana, Katibu Mkuu wa SHIMUTA, Award Safari alisema, baada ya kujitambulisha BMT, pia watakutana na Mlezi wa shirikisho hilo, Makamu wa Rais, Ali Mohamed Shein.
“Lengo ni kutaka kuutambulisha uongozi mpya uliongia madarakani baada ya uchaguzi mkuu uliofanyika mjini Tanga, ikiwa sambamba na kuelezea hali halisi ya shirikisho hilo ikiwa ni pamoja na kuiomba serikali kutoa tamko juu ya taasisi kushiriki michezo,” alisema.
Award alisema baadhi ya taasisi zimekuwa hazishiriki katika michezo hiyo baada ya kupitishwa kwa sera ya serikali ya ubinafsishaji wa mashirika ya umma, ambako amewataka kuacha kuchulia suala hilo kama kigezo cha kutoshiriki.
“Tangu baadhi ya mashirika yabinafsishwe kumekuwa na muitikio mdogo wa kushiriki, sasa tulikuwa tumepanga tukutane na serikali ili, walisisitizie jambo hilo kwani michezo katika kazi ni njia mojawapo ya ufanisi,” alisema
Maoni
Jina
Barua Pepe